Mfahamu Alfonce Innocent Haule, mtunzi wa nyimbo za Kanisa Katoliki. Kutoka Jimbo la Mbulu Parokia ya Magugu
Idadi ya nyimbo SMN: 1 > Zitazame
Jimbo analofanya utume: Mbulu
Parokia anayofanya utume: Magugu
Namba ya simu: 0784395950
Soma Historia na maelezo yake hapa
Nilizaliwa Mwaka 1968 Mkoani Kilimanjaro, Nimesoma shule za; Moshi Primary (Elimu ya Msingi), Uru Seminary (Elimu ya sekondari), MATI - UKIRIGURU; Mwanza & LITI - MPWAPWA; Dodoma (Cheti cha Kilimo na Mifugo), LITI - TENGERU; Arusha. (Diploma ya Afya na tiba ya Mifugo), na SUA - Morogoro (BSc. na MSc. Sayansi ya Mifugo).
Nilipata Elimu ya Mziki nikiwa nasoma katika Seminary ya shirika la Mitume wa Yesu (Apostles of Jesus) Uru - Moshi.
Nimeimba kwaya za Mt. Josefu Mfanyakazi Parokia ya Magugu, Babati, Mt. Josefu Mfanyakazi St. Theresia Cathedral (Arusha), Mt. Gregory Mkuu Parokia ya MODECO - Morogoro na Kwaya ya Mt. Cesilia St. Patrice Cathedral.
Ninafanya kazi Halmashauri ya Wilaya ya Babati kama Afisa Ugani Mifugo wa Wilaya.
Nimeoa na nina watoto 4 (Innocent, Anagift, Gladness na Glory)
Mungu aendelee kutuwezesha katika kazi ya Kumtumikia. AMINA.