Mtunzi: Evaristo Mfanyakazi
Makundi Nyimbo: Miito
Umepakiwa na: Joseph Isaya Mwakapila
Umepakuliwa mara 5 | Umetazamwa mara 12
Download Nota
Maneno ya wimbo
Kiitikio; Bwana ninakuja kwako mimi mwana wa mjakazi wako; uliyenitwaa kutoka katika kizazi kile dhaifu.
Ninakuomba Bwana wangu nipe neema zako (Bwana), nikatangaze neno lako kwa mataifa x 2
-
Ee Bwana umenipima ukanijua mimi, ninavyoketi na ninavyosimama mimi, ukaniweka (mimi) panapo nafasi.
-
Nilipoangushwa chini nao wabaya wangu, hukuniacha mimi mwanao niangamie, ukanishika (mkono) na kuniokoa.
-
Adui zangu walipotaka niaibike, Bwana hukuwapa nafasi ya kufanya hivyo, ukaharibu (mawazo) yao mabaya.
-
Hakika Bwana wewe u karibu na wanyonge, huwahifadhi wote waliopondeka moyo, huwafariji (walio) kata tamaa.