Ingia / Jisajili

Ee Baba Mikononi Mwako

Mtunzi: E. Kalluh
> Tazama Nyimbo nyingine za E. Kalluh

Makundi Nyimbo: Juma Kuu | Kwaresma

Umepakiwa na: Thomas George Mwakimata

Umepakuliwa mara 4 | Umetazamwa mara 61

Wimbo huu unaweza kutumika:
- Katikati Ijumaa Kuu

Download Nota (TZS 20) Download Midi
Maneno ya wimbo

Nimekukimbilia we Bwana nisiaibike milele ee Baba mikononi mwako naiweka roho yangu

1. Umenikomboa ee Bwana Mungu wa kweli/ Ee Baba mikononi mwako naiweka roho yangu.

2. Kwa sababu ya watesi wangu nimekuwa laumu/ Naam hasa kwa jirani zangu.

3. Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu/ walioniona njiani walinikimbia.

4. Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa/ Nimekuwa kama chombo kilichovunjika.

5. Maana nimesikia masingizio ya wengi/ Hofu ziko pande zote.

6. Lakini mimi nakutumaini wewe Bwana/ Nimesema, wewe ndiwe Mungu wangu.

7. Nyakati zangu zimo mikononi mwako/ Uniponye na adui zangu,nao wanaonifuatia


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa