Ingia / Jisajili

Fumbo La Kukupendeza

Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama

Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo

Umepakiwa na: Beatus Idama

Umepakuliwa mara 3 | Umetazamwa mara 44

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

FUMBO LA KUKUPENDEZA

1. Mungu Baba pokea sadaka vyetu leo, tukutoleavyo kwa jina la Mwanao; Ya Abeli na Ibrahim ilikupendeza, yetu Baba ipendeze ipokee tu.

Ipokee (ipokee) sadaka yetu, ndilo fumbo (ndilo fumbo) la kukupendeza; //: La Baba na Mwana na Roho Mtakatifu://

2. Njoni wote tutoe sadaka yetu leo, kwa sifa na utukufu wake Mwenyezi, Mkate huu na divai ndio mwili wake, kwa heshima kuu sadaka tumtolee.

3. Kama mwanzo Mungu Baba a-si-fi-we, na Mwanaye ndiye aliyetukomboa, Roho Mtakatifu ndiye wetu Mfariji, Utatu Mtakatifu Mungu mmoja twakiri.


Maoni - Toa Maoni

Janeth Alex Aug 01, 2018
jina la wimbo kwa audio unaitwaje nahitaji kuupakua youtube

george lugalinda Jul 04, 2017
Hongera nyingi natoa kwa mtunzi,kwani mm Hupenda nyimbo za zamani zinanikosha.

Toa Maoni yako hapa