Maneno ya wimbo
JIVIKENI UPENDO [E.D.MUTURA]
Jivikeni upendo, jivikeni, jivikeni upendo (upendo) ndio kifungo cha ukamilifu (ndio), ndio kifungo cha ukamilifu (ndio) ndio kifungo cha ukamilifu x2
-
Basi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu upole na uvumilivu, mkichukuliana na kusameheana.
-
Pia mtu ye yote akiwa na sababu, ya kumlaumu mwenzake, kama Bwana alivyowasamehe ninyi nyote, vivyo hivyo na ninyi nyote vumilianeni, mkichukuliana na kusameheana.
-
Na amani ya Kristo, iamue mioyoni mwenu, ndiyo mliyoitiwa, katika mwili mmoja, tena iweni watu wa shukrani kwa Bwana.
-
Neno lake Bwana likae kwa wingi, ndani yenu, katika hekima yote,mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, pia na nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia Mungu mioyoni mwenu.
-
Na kila mfanyalo kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa Yeye.