Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama
Makundi Nyimbo: Mwanzo
Umepakiwa na: Beatus Idama
Umepakuliwa mara 6 | Umetazamwa mara 34
Download Nota
Macho yangu humwelekea Bwana daima, naye atanitoa miguu yangu katika wavu, katika wavu;
(Uniangalie na kunifadhili maana mimi ni mkiwa na mteswa, maana mimi ni mkiwa na mteswa) x 2
1.Shida za moyo wangu zimeongezeka, niokoe kutoka katika dhiki yangu; Uangalie mateso na shida zangu, niondolee dhambi zangu, niondolee dhambi zangu zote.
2. Bwana nionyeshe, nionyeshe njia zako, niongoze kwenye kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe Mungu ndiwe Mwokozi wangu, tumaini langu ni kwako, tumaini langu kwako siku zote.
3.Bwana ukumbuke rehema zako, ukumbuke na upendo wako kwani zimekuwa tangu zamani; Usizikumbuke dhambi na ujana wala maasi yangu, sawasawa na upendo wako nikumbuke kwani wewe ni mwema.