Ingia / Jisajili

Mimi Ni Mtumishi Wake Bwana

Mtunzi: Fr. Gregory F. Kayeta
> Tazama Nyimbo nyingine za Fr. Gregory F. Kayeta

Makundi Nyimbo: Majilio | Mama Maria

Umepakiwa na: Vusile Silonda

Umepakuliwa mara 21 | Umetazamwa mara 42

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Mimi ni mtumishi wake Bwana, nitendewe ulivyonena x 2
Nitendewe, ulivyonena, mimi ni mtumishi wa Bwana, mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena

  1. Salamu uliyejaa neema, Bwana yu pamoja nawe.
     
  2. Usiogope Maria, Mungu kakupendelea.
     
  3. Tazama utapata mimba utamzaa mwana, utamwita jina lake Yesu.
     
  4. Huyu atakuwa mkuu, ataitwa mwana wa aliye juu.
     
  5. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi, cha Baba yake Daudi.
     
  6. Ataitawala nyumba ya Yakobo hata milele, ufalme wake hautakuwa na mwisho.
     
  7. Roho Mtakatifu atakushukia, na nguvu ya yule aliye juu itakutia kivuli.
     
  8. Ndiyo maana huyo mtoto atakuwa mtakatifu, huyo ataitwa mwana wa Mungu.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa