Ingia / Jisajili

Mmeuvua Kabisa Utu Wa Kale

Mtunzi: Frt. Peter L. Ndayisaba
> Tazama Nyimbo nyingine za Frt. Peter L. Ndayisaba

Makundi Nyimbo: Mafundisho / Tafakari

Umepakiwa na: Peter Leonard Ndayisaba

Umepakuliwa mara 8 | Umetazamwa mara 27

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

                                                                MMEUVUA KABISA UTU WA KALE

(K)Mmeuvua (kabisa) utu wa kale, pamoja na matendo yake; mkivaa utu mpya,unaofanywa upya upate ufahamu (sawasawa) sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.

                                                                                 Mashairi

1. Basi, vifisheni vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi: uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu; kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu.

2. Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote: hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu. msiabiane uongo, kwa kuwa mmeuvua kabisa utu wa kale.

3. Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa Rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, mkichukuliana na kusameheana, mtu akiwana sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

4. Neno la Kristu na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu. Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu baba kwa yeye.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa