Ingia / Jisajili

Msaada Wangu

Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Beatus Idama

Umepakuliwa mara 13 | Umetazamwa mara 41

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

MSAADA WANGU U KATIKA BWANA

Msaada wangu u katika Bwana, msaada wangu u katika Bwana
aliyezifanya mbingu na nchi, aliyezifanya mbingu na nchi;
Msaada wangu u katika Bwana

1. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu, Israeli na aseme sasa; kama Bwana asingalikuwa upande wetu muda ule watu walipotushambulia; Wakati hasira yao ilipokuwa dhidi yetu, wangalitumeza, wangalitumeza tukiwa hai.

2. Bwana atakulinda, yeye ni uvuli wa mkono wako, ni uvuli wa mkono wako wa kuume; jua halitakudhuru mchana wala mwezi hautakudhuru wakati wa usiku; Bwana atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako maisha yako.

3. Bwana na asifiwe, yeye hakuruhusu turaruriwe na meno yao, Tumeponyoka kama ndege kutoka katika mtego wa mwindaji; mtego umevujika na sisi tumeokoka, mtego umevunjika nasi tumeokoka.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa