Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama
Makundi Nyimbo: Zaburi
Umepakiwa na: Beatus Idama
Umepakuliwa mara 13 | Umetazamwa mara 41
Download Nota Download MidiMSAADA WANGU U KATIKA BWANA
Msaada wangu u katika Bwana, msaada wangu u katika Bwana
aliyezifanya mbingu na nchi, aliyezifanya mbingu na nchi;
Msaada wangu u katika Bwana
1. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu, Israeli na aseme sasa; kama Bwana asingalikuwa upande wetu muda ule watu walipotushambulia; Wakati hasira yao ilipokuwa dhidi yetu, wangalitumeza, wangalitumeza tukiwa hai.
2. Bwana atakulinda, yeye ni uvuli wa mkono wako, ni uvuli wa mkono wako wa kuume; jua halitakudhuru mchana wala mwezi hautakudhuru wakati wa usiku; Bwana atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako maisha yako.
3. Bwana na asifiwe, yeye hakuruhusu turaruriwe na meno yao, Tumeponyoka kama ndege kutoka katika mtego wa mwindaji; mtego umevujika na sisi tumeokoka, mtego umevunjika nasi tumeokoka.