Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama
Makundi Nyimbo: Zaburi
Umepakiwa na: Beatus Idama
Umepakuliwa mara 4 | Umetazamwa mara 40
Download Nota Download MidiMSIFUNI BWANA HUWAPONYA WALIOPONDEKA MOYO
//:Msifuni Bwana huwaponya waliopondeka moyo, msifuni Bwana huwaponya waliopondeka moyo://
1. Ee nafsi yangu umsifu Bwana, nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu ningali hai, ningali hai, ningali hai.
2. Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa; roho zao hrudi mavumbini, mipango yao siku hiyo hukoma.
3. Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake; ambaye tumaini lake ni Bwana Mungu wake, muumba wa mbingu na dunia, bahari na vyote vilivyomo; ni mwaminifu milele na milele.
4. Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote na mwenye upendo kwa vitu vyote alivyovifanya; Bwana yu karibu kwa wote wamwitao, wamwitao kwa uaminifu.