Ingia / Jisajili

Msifuni Bwana Huwaponya Waliopondeka Moyo

Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama

Makundi Nyimbo: Zaburi

Umepakiwa na: Beatus Idama

Umepakuliwa mara 4 | Umetazamwa mara 40

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

MSIFUNI BWANA HUWAPONYA WALIOPONDEKA MOYO

//:Msifuni Bwana huwaponya waliopondeka moyo, msifuni Bwana huwaponya waliopondeka moyo://

1. Ee nafsi yangu umsifu Bwana, nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu ningali hai, ningali hai, ningali hai.

2. Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa; roho zao hrudi mavumbini, mipango yao siku hiyo hukoma.

3. Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake; ambaye tumaini lake ni Bwana Mungu wake, muumba wa mbingu na dunia, bahari na vyote vilivyomo; ni mwaminifu milele na milele.

4. Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote na mwenye upendo kwa vitu vyote alivyovifanya; Bwana yu karibu kwa wote wamwitao, wamwitao kwa uaminifu.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa