Maneno ya wimbo
Kiimbilizi
1. Tunakushukuru Mungu Baba twakushukuru, kwa kulijalia kanisa mtumishi wako twashukuru.
Kiitikio:
Festo mwana wa Kitosi - Hongera baba Kitosi, Mungu amekuchagua kati ya wengi, Karibu baba Kitosi - Karibu kwetu nyumbani, tumshukuru Mwenyezi kwa pamoja.x2
2. Mungu akulinde ujaliwe baraka tele, utimize vema kazi yako kwa wokovu wa watu wote
3. Uwachunge vema kondoo wasije potea, tafuta waliopotea warudi nyumbani kwake Baba.
4. Hongera hongera hongera tunakupongeza, kaifanye kazi kwa sifa mtukuze Mungu sikuzote
Kimalizio cha shangwe:
Tufurahi leo wote tumsifu Mungu - A le lu ya tunaimba, heko baba Kitosi kwa daraja takatifu - hongera baba hongera..