Mtunzi:
Makundi Nyimbo: Sadaka / Matoleo
Umepakiwa na: Joseph Mitepa
Umepakuliwa mara 0 | Umetazamwa mara 2
Download Nota Download Midi1.Tupeleke vipaji vyetu ( vipaji ) vipaji tulivyoviandaa, tupeleke na nafsi zetu mapato yetu tumpe Bwana,
Tupeleke na fedha zetu (na fedha) na fedha tulizoziandaa,tukatoe na mali zetu mifugo yetu tumpe Bwana.
2.Ipokee sadaka yetu (sadaka) sadaka tunayakutolea,zipokee na sala zetu maombi yetu uyapokee,
Upokee matoleo yetu (Ee Bwana) zawadi tunazokutolea, upokee uzima wetu na dhambi zetu uzitakase.
3.Tupeleke mazao yetu (mazao) mazao aliyotujalia, tupeleke nafaka zetu na ngano zetu tumpe Bwana,
Tupekeke divai yetu (divai) divai tunda la mzabibu, tukatoe mkate wetu viigeuzwe mwili na damu.
4.Tukatoe shukrani zetu (shukrani) uhai aliotujalia, tuyatoe maisha yetu elimu yetu tumpe Bwana,
Tupokee baraka yake (baraka) baraka anayotubariki, tupokee na neema zake na nguvu zake toka kwa Bwana.
5.Tupeleke na shida zetu (na shida) na shida zinazotuandama, tupeleke maradhi yetu magonjwa yetu tumpe Bwana,
Tupeleke mateso yetu (mateso) ya vita vinavyotuandama, tupeleke tulivyonavyo kwa imani tutazidishiwa.