Ingia / Jisajili

Uliomegwa Kwa Ajili Ya Wote

Mtunzi: Fr. Amadeus Kauki
> Tazama Nyimbo nyingine za Fr. Amadeus Kauki

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio

Umepakiwa na: Yudathadei Chitopela

Umepakuliwa mara 24 | Umetazamwa mara 77

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo
  1. Tukitazama kwa macho Eeh, twauona ni mkate.
    Lakini ndani yake Eeh, yumo Kristu Bwana wetu.

    Anakaa kwetu sisi Eeh, (kwenye) fumbo kuu takatifu la Ekaristi atulisha na kutunywesha (Bwana) chakula chenye uzima.
    Loo wema wa ajabu Eeh, (tena) ni upendo usioelezeka kwetu Mungu kutulisha mwenyewe, (tena) kwa mwili na damu yake.
     
  2. Ni mkate ulomegwa Eeh, kwa ajili yetu sote,
    Sote tupate shiriki Eeh, huo upendo wa Mungu.

    Ndo sadaka ya msalaba Eeh, (ndivyo) sadaka iliyompendeza Ba-ba, Ili tupate mastahili, (hasa) kusimama mbele zake.
    Dhambi zetu zikafutwa Eeh, (hivyo), tukapatanishwa naye Muumba we-tu,hivyo ndugu yangu Mkristu (wewe) tafakari jambo hili.
     
  3. Tujiandae kwa toba Eeh, tusafishe nyoyo zetu.
    Tujongee kwa imani Eeh, tumpokee Bwana Yesu.
     
    Bila imani ya kweli Eeh, (kweli) hatuwezi kamwe kumuona Bwa-na aliyejificha nda-ni (nda ni) ya mkate na divai.
    Sisi sote wadhaifu Eeh (hivyo) tusipojikubali na kuomba toba, tukienda kushiri-ki, (ndugu) tunapokea hukumu.
     
  4. Karibu nyoyoni mwetu Eeh, kaa nasi Bwana Yesu.
    Wewe ndiwe chemchemi Eeh, ya baraka na neema.
     
    Ni kiini cha maisha Eeh, (pia) ni mlango wa kumuendea Ba-ba, Bila wewe twaogopa Eh, (Bwana) safari ni ngumu m-no.
    Utujaze ufahamu Eeh, (tena) utuongezee imani yetu haba, Tukutambue maishani, (kwenye) shughuli za kila siku.

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa