Ingia / Jisajili

Bwana Amejaa Huruma

Mtunzi: Martin Mutua Munywoki
> Tazama Nyimbo nyingine za Martin Mutua Munywoki

Makundi Nyimbo: Mwaka wa Huruma ya Mungu | Zaburi

Umepakiwa na: Martin Munywoki

Umepakuliwa mara 7 | Umetazamwa mara 36

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Bwana amejaa huruma (na neema)

Amejaa huruma na neema, amejaa huruma na neema

1. Ee nafsi yangu umhimidi Bwana (Bwana), na vyote vilivyomo ndani yangu ndani ya-ngu

Vilihimidi Jina lake takatifu (Jina) ee ee nafsi yangu umhi-midi Bwana

Wala usizisahau fadhili zake zake zote (fadhili), Usisahau, na fadhili zake zote

2. Akusame-he maovu yako yote (yote), Akuponya magonjwa yako yote yako yote

Aukomboa uhai wako na kaburi (lako), akuti-a taji la fadhili na rehema

Bwana ndiye atendaye atendaye mambo ya haki(ya haki), na hukumu kwa wote wanaoonewa

3. Alimjulisha Musa nji-a yake (njia), nao wana wana wa Israeli matendo yake

Bwana amejaa huruma na neema (ne'ma), hakasiriki upesi ni mwingi wa fadhili

Mbingu zilivyoinuka juu ya nchi kadri ile (ileile), rehema zake, ni kuu kwa wamchao


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa