Jiandae wiki nzima weka tayari sadaka yako mkristu (toa kwa moyo safi)
Usitoe kwa uchoyo wala sadaka ya kuazima
{(jasho lako) umtolee Mungu alicho kupa hahitaji zaidi
(maana)?Vitu vyote mali yake toa kwa ukarimu } *2
1. Ninaona hasara kutoa (nanung'unika) Bwana ona nilivyochanganyikiwa
Mara nyingi naomba jirani (hapa kitini) siyo yangu ni sadaka ya kuazima
2. Ninaona uchoyo kutoa (sadaka yangu) ninaleta kidogo tena kwa uchungu
Mara nyingine sitoi kitu (nilicho nacho) ninaficha sadaka yangu mfukoni
3. Ninaona aibu kubaki (ni wasiwasi) nimeketi nao wengine wanatoa
Mara nyingine hata siendi (nimekimbia) kanisani ninahepa michango nyingi
4. Wana baraka wanaotoa (kwa moyo ule ) wa Abeli wa Ibrahimu na Isaka
Bwana Mungu haipendi sadaka (yake Kaini) wala Ana-nia na Safira