ALIDHARAULIWA NA KUKATALIWA
Alidharauliwa na kukataliwa kukataliwa na watu
Mtu mwenye huzuni nyingi ajuaye sikitiko sikitiko
1.Kwa maana alikua kama mche mwororo
Na kama mzizi katika nchi nchi kavu
Yeye hana umbo hana umbo wala uzuri
Hata tumwonapo tumtamani
Kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao
Wala hatukumhesabu yeye kuwa kitu
2.Hakika amechukua masikitiko yetu
Amejitwika huzuni zetu amejitwika
Lakini tulimdhania kuwa amepigwa
Amepigwa na Mungu na kuteswa
Bali alijeruhiwa kwa ma-kosa yetu
Alichubuliwa kwa maovu maovu yetu
3.Adhabu ya amani yetu kawa juu yake
Na kwa kupigwa kwake yeye sisi tumepona
Sisi sote kama kondoo tumepotea
Kila mmoja njia yake mwenyewe
Bwana ameweka juu yake maovu yetu
Alionewa laki-ni alinyenyekea
4.Kaonewa wala hakufunua kinywa chake
Kama mwanakondoo akipelekwa machinjoni
Kwa kuonewa kuhukumiwa kaondolewa
Ni nani atasimulia haya
Maana amekataliwa mbali nayo nchi
Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya
5.Ingawa hakutenda jeuri kinywani mwake
Lakini Bwana aliridhika kumchubua
Utakapofanya nafsiye dhabihu kwa dhambi
Ataona uzao wake yeye
Ataishi siku nyingi na mapenzi ya Bwana
Yatafanikiwa mkononi mkononi mwake