Ingia / Jisajili

Chakula Cha Watoto

Mtunzi: Martin Mutua Munywoki
> Tazama Nyimbo nyingine za Martin Mutua Munywoki

Makundi Nyimbo: Ekaristi / Komunio

Umepakiwa na: Martin Munywoki

Umepakuliwa mara 5 | Umetazamwa mara 28

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

Si sawa kuchukua chakula cha watoto (si sawa) 

Na kuwatupia mbwa chakula cha watoto (lakini)

Hata mbwa hula makombo yaangukayo (kutoka) mezani mwa Bwana wao

Nami natamani kuonja chakula hiki  (ulicho) waandalia wanao

{ Japo sifai mimi nakusihi Bwana uniruhusu tu } *2

1. Ninatamani sana, Bwana wangu (mwema), kujongea karamuni,

Ijapokuwa mimi sina moyo safi, nina njaa nina kiu niruhusu tu
 
2. Nimejawa na dhambi, na uchafu (mwingi), na nimeoza moyoni
Mawazo mabaya na matendo maovu, hata naona aibu, niruhusu tu
 
3. Nisipokupokea, mwili wako (Bwana), sina uzima milele
Sasa niende wapi zaidi ya kwako, nisamehe nipokee niruhusu tu
 
4. Maana ulikuja, duniani (kwao), wenye dhambi kama mimi
Ulikula nao hata ukafa nao, na mimi nakuhitaji niruhusu tu
 
5. Nimetenda jeuri, mtukutu (sana), amri zako nimeasi
Usinikemee kwa hasira mezani, nionee hurumayo niruhusu tu
 
 

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa