Ingia / Jisajili

Misa Ya Mt. Veronicah

Mtunzi: Martin Mutua Munywoki
> Tazama Nyimbo nyingine za Martin Mutua Munywoki

Makundi Nyimbo: Misa

Umepakiwa na: Martin Munywoki

Umepakuliwa mara 30 | Umetazamwa mara 55

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

MISA YA MTAKATIFU VERONICAH

A. EE BWANA UTUHURUMIE

Ee Bwana (Bwana Mungu) utuhurumie (ee Bwana)

ee Bwana Mungu (tuhurumie) utuhurumie (ee Bwana ee Mungu Mungu utuhurumie

Ee Yesu (Kristu) utuhurumie

Ee Yesu Kristu utuhurumie

B. UTUKUFU

Utukufu (juu) kwa Mungu Mbinguni

Na amani iwe kote duniani (tunakuabudu)

Tunakusifu Bwana twakuheshimu Bwana tunakuabudu

Twakutukuza Bwana twakuheshimu Bwana

1. Ewe Bwana Mungu Baba mfalme wa Mbinguni

Tunakushukuru kwa utukufu mkuu, Mungu Baba Mwenyezi

2. Ewe Bwana Yesu Kristu Mwana wa pekee

Mwana kondoo Mungu uondoaye dhambi, utuhurumi-e

3. Uondoaye dhambi zetu  utusikie,

Ewe uketiye kuume kwa Mungu Baba, utuhurumi-e

4. U pekee Bwana  Mtakatifu na u Kristu

Pamoja naye Roho katika utukufu, wake Mungu milele

C. ALELUYA

Aleluya (aleluya) aleluya (aleluya) aleluya aleluya

D. NASADIKI

Nasadiki (kwa Mungu Baba),

nasadiki (kwa Mungu Mwana)

Nasadiki (kwa Mungu Roho) nasadiki

1. Nasadiki kwa Mungu mmoja Baba ye-tu Mwenye-zi

Nasadiki Yesu Kristu mwana wake wa pekee

Nasadiki alipata mwili kwa Roho Mtakati-fu

Nasadiki kazaliwa na Bikira Maria

2. Aliteswa alisulubiwa kwa amri ya Pnsyo Pilato

Akafa na akazikwa na kushuka kwa wafu

Alifufuka siku ya tatu na kupaa juu Mbingu-ni

Toka huko tarudi kuhukumu ulimwengu

3. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu na Kanisa Katoliki

Nasadiki Ushirika wao Watakatifu

Nasadiki ufufuko wa miili na ondoleo la dhambi

Nasadiki uzima wa milele na milele

E. MTAKATIFU

Mtakatifu (Bwana Mungu) Mtakatifu (wa Majeshi) *2

Mbingu na dunia zimejaa zimejaa

Zimejaa utukufu wako Bwana

{Hosanna juu Mbinguni Hosanna Mbinguni juu Hosanna juu } *2

Amebarikiwa amebarikiwa yeye

Yeye ajaye kwa jina lake Bwana

F. FUMBO LA IMANI

Yesu Kristu alikufa Yesu alifufuka

Atarudi Yesu atakuja tena

G. AMINA

Amina (amina) amina (amina) amina amina

H. BABA YETU

1. Baba Yetu uliye Mbinguni, jina lako litukuzwe daima

Na ufalme wako na ufike na mapenzi yako yatimilike

Utakalo (utakalo) lifanyike (lifanyike) duniani (duniani) kama Mbinguni *2

2. Tupe leo na mkate wetu, tupe mkate wetu wa kila siku

Tusamehe na makosa yetu,  vile tusameheavyo wengine

3. Situtie vishawishi-ni, bali utuopoe maovuni

Situtie vishawishi-ni, bali utuopoe maovuni

4. Kwa maana ufalme ni wako, na nguvu pia nao utukufu

Kwa maana ufalme ni wako, na nguvu pia nao utukufu

 I. MWANA KONDOO WA MUNGU

  1. Ee Mwana Kondoo wa Mungu,
    Unayeziondoa dhambi za dunia (dhambi zote za dunia)
    Tuhurumie (tuhurumie) utuhurumie
  2. Ee Mwana Kondoo wa Mungu,
    Unayeziondoa dhambi za dunia (dhambi zote za dunia)
    Tuhurumie (tuhurumie) utuhurumie
  3. Ee Mwana Kondoo wa Mungu,
    Unayeziondoa dhambi za dunia (dhambi zote za dunia)
    Tupe amani (tupe amani) utupe amani

Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa