Mtunzi: Martin Mutua Munywoki
> Tazama Nyimbo nyingine za Martin Mutua Munywoki
Makundi Nyimbo: Misa
Umepakiwa na: Martin Munywoki
Umepakuliwa mara 30 | Umetazamwa mara 55
Download Nota Download MidiEe Bwana (Bwana Mungu) utuhurumie (ee Bwana)
ee Bwana Mungu (tuhurumie) utuhurumie (ee Bwana ee Mungu Mungu utuhurumie
Ee Yesu (Kristu) utuhurumie
Ee Yesu Kristu utuhurumie
Utukufu (juu) kwa Mungu Mbinguni
Na amani iwe kote duniani (tunakuabudu)
Tunakusifu Bwana twakuheshimu Bwana tunakuabudu
Twakutukuza Bwana twakuheshimu Bwana
1. Ewe Bwana Mungu Baba mfalme wa Mbinguni
Tunakushukuru kwa utukufu mkuu, Mungu Baba Mwenyezi
2. Ewe Bwana Yesu Kristu Mwana wa pekee
Mwana kondoo Mungu uondoaye dhambi, utuhurumi-e
3. Uondoaye dhambi zetu utusikie,
Ewe uketiye kuume kwa Mungu Baba, utuhurumi-e
4. U pekee Bwana Mtakatifu na u Kristu
Pamoja naye Roho katika utukufu, wake Mungu milele
Aleluya (aleluya) aleluya (aleluya) aleluya aleluya
Nasadiki (kwa Mungu Baba),
nasadiki (kwa Mungu Mwana)
Nasadiki (kwa Mungu Roho) nasadiki
1. Nasadiki kwa Mungu mmoja Baba ye-tu Mwenye-zi
Nasadiki Yesu Kristu mwana wake wa pekee
Nasadiki alipata mwili kwa Roho Mtakati-fu
Nasadiki kazaliwa na Bikira Maria
2. Aliteswa alisulubiwa kwa amri ya Pnsyo Pilato
Akafa na akazikwa na kushuka kwa wafu
Alifufuka siku ya tatu na kupaa juu Mbingu-ni
Toka huko tarudi kuhukumu ulimwengu
3. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu na Kanisa Katoliki
Nasadiki Ushirika wao Watakatifu
Nasadiki ufufuko wa miili na ondoleo la dhambi
Nasadiki uzima wa milele na milele
Mtakatifu (Bwana Mungu) Mtakatifu (wa Majeshi) *2
Mbingu na dunia zimejaa zimejaa
Zimejaa utukufu wako Bwana
{Hosanna juu Mbinguni Hosanna Mbinguni juu Hosanna juu } *2
Amebarikiwa amebarikiwa yeye
Yeye ajaye kwa jina lake Bwana
Yesu Kristu alikufa Yesu alifufuka
Atarudi Yesu atakuja tena
Amina (amina) amina (amina) amina amina
1. Baba Yetu uliye Mbinguni, jina lako litukuzwe daima
Na ufalme wako na ufike na mapenzi yako yatimilike
Utakalo (utakalo) lifanyike (lifanyike) duniani (duniani) kama Mbinguni *2
2. Tupe leo na mkate wetu, tupe mkate wetu wa kila siku
Tusamehe na makosa yetu, vile tusameheavyo wengine
3. Situtie vishawishi-ni, bali utuopoe maovuni
Situtie vishawishi-ni, bali utuopoe maovuni
4. Kwa maana ufalme ni wako, na nguvu pia nao utukufu
Kwa maana ufalme ni wako, na nguvu pia nao utukufu