Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama
Makundi Nyimbo: Majilio
Umepakiwa na: Beatus Idama
Umepakuliwa mara 8 | Umetazamwa mara 62
Download Nota Download MidiEE BWANA NAKUINULIA NAFSI YANGU
Ee Bwana ee Bwana nakuinulia nafsi yangu ee Mungu wangu, nimekutumaini wewe nisiaibike;
Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda, adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.
1. Naam wakungojao hawataaibika, hawataaibika, hawataaibika hata mmoja, wataaibika wale wote wakuasio, wakuasio Bwana kwa makusudi.
2. Unijulishe njia zako ee Bwana, unifundishe mapito yako uniongoze katika kweli, kweli yako, kwani wewe ni Mungu pia Mwokozi wangu nakutegemea wewe kila siku.
3. Uzikumbuke rehema zako ee Bwana, na ukumbuke fadhili zako kwa maana zimekuwako toka zamani,usikumbuke dhambi za ujana wangu nikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako.