Ingia / Jisajili

Familia Takatifu - Wajibu Na Fadhila

Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama

Makundi Nyimbo: Anthem

Umepakiwa na: Beatus Idama

Umepakuliwa mara 7 | Umetazamwa mara 62

Download Nota Download Midi
Maneno ya wimbo

FAMILIA TAKATIFU - WAJIBU NA FADHILA

Ni mpango wa Mungu viumbe wake tuishi katika familia

Familia ni kanisa, kanisa la nyumbani la Baba, Mama na Watoto

//Familia ya Wakristu yapaswa kuishi kikristu, kuuishi wajibu wake na kuziishi fadhila zake, hapo hujidhihirisha utakatifu wa familia kama familia ile ya Yesu, Maria na Baba Yosefu//

Hivyo wazazi tuwalee watoto kimwili na kiroho - nao wamjue Mungu waongee naye kwa sala na matendo mema;

Wawe wenye heshima, watii na wenye kujali - wenye msaada ili wakue kimo na busara

Wajue kusali, mkumsifu na kumcha Mungu - wakue imani ili wampendeze Mungu

//Upendo, uvumilivu na msamaha: Upendo, uvumilivu na msamaha ni fadhila, ni fadhila za familia takatifu//

Haya yote tunayaiga toka ile Familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefu.


Maoni - Toa Maoni

Hakuna maoni kwenye wimbo huu

Toa Maoni yako hapa