Mtunzi: Beatus M. Idama
> Tazama Nyimbo nyingine za Beatus M. Idama
Makundi Nyimbo: Anthem
Umepakiwa na: Beatus Idama
Umepakuliwa mara 7 | Umetazamwa mara 62
Download Nota Download MidiFAMILIA TAKATIFU - WAJIBU NA FADHILA
Ni mpango wa Mungu viumbe wake tuishi katika familia
Familia ni kanisa, kanisa la nyumbani la Baba, Mama na Watoto
//Familia ya Wakristu yapaswa kuishi kikristu, kuuishi wajibu wake na kuziishi fadhila zake, hapo hujidhihirisha utakatifu wa familia kama familia ile ya Yesu, Maria na Baba Yosefu//
Hivyo wazazi tuwalee watoto kimwili na kiroho - nao wamjue Mungu waongee naye kwa sala na matendo mema;
Wawe wenye heshima, watii na wenye kujali - wenye msaada ili wakue kimo na busara
Wajue kusali, mkumsifu na kumcha Mungu - wakue imani ili wampendeze Mungu
//Upendo, uvumilivu na msamaha: Upendo, uvumilivu na msamaha ni fadhila, ni fadhila za familia takatifu//
Haya yote tunayaiga toka ile Familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefu.